Psalms 72:1-5
Maombi Kwa Ajili Ya Mfalme
(Zaburi Ya Sulemani)
1 aEe Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako,
mwana wa mfalme kwa haki yako.
2 bAtawaamua watu wako kwa haki,
watu wako walioonewa kwa haki.
3 Milima italeta mafanikio kwa watu,
vilima tunda la haki.
4 cAtawatetea walioonewa miongoni mwa watu
na atawaokoa watoto wa wahitaji,
ataponda mdhalimu.
5 dAtadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.
Copyright information for
SwhKC